Tunajenga lugha ya kupanga kwa Kiswahili, kwa jamii ya wasanidi wa Afrika ya Mashariki na dunia nzima. Kila mshiriki anastahili heshima, bila kujali asili, lugha, uzoefu au mtazamo.
- Lugha ya mawasiliano ya mradi ni Kiswahili. Kama Kiswahili chako si kikamilifu, mchanganyiko unaoeleweka unakubalika — kujifunza ni sehemu ya jamii hii.
- Kosoa kazi, si mtu. Mende ni ya msimbo, si ya mwandishi.
- Wageni wanakaribishwa. Swali lolote la kwanza ni mchango halali.
Kanuni za maadili za kina ziko kwenye hazina ya Swa: lugha-swa/swa/CODE_OF_CONDUCT.md
Ripoti kwa barua pepe ya usalama iliyoorodheshwa kwenye lugha-swa/swa/SECURITY.md. Ripoti zinashughulikiwa kwa siri.